Friday 27 January 2017

Angalia Data za World Bank; Nani Zaidi - Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli Kwa Uchumi Tanzania



Labda hiyo grapgh haoinekani vizuri, lakini inachoonyesha ni kwamba kulingana na data za Benki ya dunia, tukitumia GDP per capital growth rate, katika kipindi cha Mwinyi, Mkapa na JK, Mkapa ndio aling'ara kwenye kuinua ukuzi wa uchumi, tunapolinganisha alipoingia na alipotoka, na kwa ujumla.

Japo kwa Mwinyi tunachoona ni miaka yake mitano ya mwisho - inaonyesha aliuacha uchumi katika hali mbaya kuliko kipindi chake cha kwanza cha miaka mitano. Mwinyi peke yake aliingiza Tanzania kwenye negative GDP per capital growth rate, hadi wastani wa -3%.

Mkapa alipochukua nchi aliuboresha uchumi zaidi sana ya Mwinyi alipouacha. Kuelekea mwishoni mwa kipindi cha Mkapa kasi ya ukuzi ilipungua, labda ni kipindi kila mtu alianza kuchukua chake! Kwa ujumla ukuzi wa uchumi wakati wa Mkapa ulikuwa na msimamo mzuri unaoeleweka, sio panda shuka ya Mwinyi na Kikwete.

Kikwete alipochukua toka kwa Mkapa ghafla uchumi alianza kuporoka chini zaidi ya pale alipouacha Mkapa. Jambo lililo wazi ni kwamba wakati wa Kikwete ukuzi wa uchumi ulikuwa hauna msimamo kamili, kila mwaka kupanda na kushuka kuonyesha Kikwete hakuwa na mwelekeo unaoeleweka katika mambo ya uchumi ukilinganisha na Mkapa. Kwa wastani Kikwete aliushusha uchumi kuliko alipouacha Mkapa.

Katika kipindi cha mwaka mmoja cha JPM, japo watu wanalalamika kwamba shilingi imeota miguu, lakini yeye amefikia rekodi ya GDP per capita growth rate ambayo haijawahi kufikiwa na maraisi wote waliomtangulia. Magufuli alipochukua tu nchi toka kwa Kiwete tulianza kupanda. Sasa hii inamaanisha nini kuelekea mbele tunasubiri kuona, na mwishoni mwa 2017 tutapata picha kamili.

Ila picha ya ujumla ni kwamba tangu 1990 hadi 2016 tumeenda vizuri sana. Katika kipindi cha Mwinyi na Kikwete kwa wastani hatukwenda mbele wala kurudi nyuma. Hadi sasa ni Mkapa peke yake aliyetuinua tangu mwaka 1990. Na Magufuli anaonekana ana mwelekeo wa kutuinua toka pale alipotuacha Mkapa.

NB. Data za 2016 kipindi cha JPM hapo juu ni halisi, isipokuwa zimefanywa wastani wa quarter tatu (January - September), Q1, Q2, Q3, badala ya nne za miaka mingine.

Source: GDP per capita growth (annual %) | Data

GHARAMA ZA UNGA

Wewe kama mjasiriamali au mfanya biashara unatumiaje fursa ya kupanda kwa gharama za biashara mbalimbali kuanzisha biashara yako??

Tuachie maoni yako tafadhari..

au wasiliana nasi kwa ushauri zaidi 0766865041



Hali mbaya: Makampuni ya simu yaanza kupunguza wafanyakazi. ITV yasogeza mishahara mbele

Hali tumbua majipu na kuzuia pesa za ovyo yazidi kuumiza vichwa watu hadi makampuni makubwa ya simu..


UTARATIBU WA WAJASIRIAMALI WADOGO NA WA KATI (SMEs) KUWEZESHWA KUPATA ALAMA YA UBORA YA ‘TBS’

kumbuka kuwasiliana nasi kwa ushauri zaidi 0766865041


1.0 UTANGULIZI

Serikali hutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya kuhudumia wajasiriamali wadogo na wa kati pale wanapoomba bidhaa zao wanazozizalisha wenyewe zithibitishwe ubora. Katika utaratibu huu, wapo wajasiriamali ambao husamehewa kulipa ada yoyote kwa sababu ya mitaji yao kuwa midogo.
Ili kupata msamaha huu, vigezo vifuatavyo huzingatiwa:

 Mjasiriamali hutakiwa kuwa na barua ya utambulisho kutoka ofisi ya SIDO iliyo karibu. Ni vema kuhakikisha kuwa barua inafafanua vizuri na kwa kina shughuli zinazofanywa.
 Kwa wale wanaozalisha vyakula huhitajika kuwa na taarifa fupi kutoka Idara ya Afya iliyo karibu na mahali pa uzalishaji au cheti cha TFDA.
 Mjasiriamali hupaswa kuwa na leseni ya biashara.
 Wajasiriamali waliokwishapata leseni ya kutumia alama ya ubora hupaswa kutunza rekodi za uzalishaji na mauzo ambazo watatakiwa kuzionesha kwa wakaguzi wa TBS pindi zinapohitajika.

2.0 HATUA ZA KUPATA ALAMA YA UBORA YA ‘tbs’

2.1 HATUA YA KWANZA – MAOMBI

i) Maombi ya uthibitishaji wa ubora wa bidhaa hufanywa na mwombaji kwenda kwa Mkurugenzi Mkuu wa TBS kwa maandishi.
ii) Majibu hutolewa yakielezea taratibu na gharama zote.
iii) Majibu huambatana na fomu maalum ambayo mwombaji huijaza na kuirudisha TBS ikiwa na viambatanisho vifuatavyo:
• Mtiririko wauzalishaji wa bidhaa husika;
• Mfumo wa uongozi ukionyesha kitengo cha udhibiti ubora;
• Orodha ya malighafi anazotumia na mahali zinakotoka kwa kila bidhaa;
• Ramani inayoelekeza jinsi ya kufika kiwandani kwako;
Baada ya hapo tarehe ya kufanya ukaguzi wa awali hupangwa.

2.2 HATUA YA PILI – UKAGUZI WA AWALI

• Ukaguzi wa awali hufanywa na wakaguzi wa TBS wa kati kiwanda kikiwa katika uzalishaji.
• Sampuli huchukuliwa na kupimwa ili kuona kama zinakidhi matakwa ya kiwango husika.
• Mkaguzi huandaa taarifa kuhusu hali halisi ya kiwanda na mambo yanayostahili kurekebishwa.
2.3HATUA YA TATU – UPIMAJI

• Sampuli zilizochukuliwa hupimwa katika maabara za TBS kwa kufuata kiwango husika.
• Baada ya kazi ya upimaji kumalizika, ripoti ya maabara hutolewa kwa mwombaji.

2.4 HATUA YA NNE – UTOAJI WA LESENI

• Maamuzi kuhusu kutoa au kutotoa leseni ya kutumia alama ya ubora hutegemea tu ripoti ya ukaguziwa awali wa kiwanda pamoja na ripoti ya maabara.
• Kimsingi ripoti zote mbili zinatakiwa kuonyesha kwamba mazingira ya uzalishaji kiwandani, mfumo wauzalishaji na bidhaa iliyopimwa havina matatizo.
• Ikiwa sivyo basi mzalishaji hutakiwa kufanya marekebisho na baadaye mkaguzi wa TBS hutumwa tena na kuleta sampuli nyingine.

3.0 MUDA WA LESENI (VALIDITY OF LICENCE) YA ALAMA YA UBORA YA ‘tbs’


Leseni ya kutumia alama ya ubora ya ‘tbs’ hudumu kwa mwaka mmoja na huhuishwa (renewal) baada ya kuhakikisha kwamba taratibu zilizokubalika (Scheme of Inspection and Test, SIT) zinafuatwa.

AINA ZA MUUNDO WA BIASHARA

kumbuka kuwasiliana nasi kwa ushauri zaidi 0766865041

Utangulizi
Mojawapo ya maamuzi ya mwanzoni kabisa unayohitaji kufanya kwa ajili ya biashara yako mpya ni kuchagua aina ya muundo wa biashara unaoona unakufaa. Uchaguzi unaofanya ni muhimu kwa kuwa utaathiri uwezo na mamlaka ya biashara yako kufanya au kutofanya jambo fulani. Kuwa na aina na muundo sahihi wa biashara kutakusaidia kukuongoza wakati biashara yako iko kwenye mafanikio au wakati wa taabu.
Muundo sahihi wa biashara ndio utakuongoza nini cha kufanya ikiwa utashtakiwa, na kwa namna gani wewe na biashara yako mtatozwa kodi. Kimsingi ziko namna kuu tatu za kuunda biashara, zimeelezewa hapa chini
Biashara inayoendeshwa na mtu binafsi peke yake
Biashara inayomilikiwa na kuendeshwa kwa Ubia
Kampuni yenye ukomo wa madeni
Biashara inayomilikiwa/ kuendeshwa na mtu mmoja
Biashara inayoendeshwa na mtu binafsi peke yake, au Mfanyabiashara pekee ni aina ya biashara ambayo imeenea sana miongoni mwa wajasiriamali nchini. Hii ni biashara ambayo ni rahisi sana kuanzisha kwani mmiliki hufanya usajili wa jina la biashara na kutimiza masharti mengine machache kabla ya kufungua bishara.
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) imetoa mwongozo wa kusajili jina la biashara ambapo mjasiriamali atatakiwa kulipia wastani wa Shilingi 20,000. Mwongozo huu unapatikana kwenye tovuti ya Brela. Mada zijazo pia tutajadili namna ya kusajili biashara.

Biashara inayomilikiwa na mtu mmoja inaweza kuendeshwa kwa jina la mmiliki au jina jingine lisilo lake. Biashara ya aina hii imejipatia umaarufu mkubwa sana kutokana na urahisi wake, haswa katika uanzishaji, pamoja na gharama ndogo. Mfanyabiashara anahitaji tu kujisajili au kusajili jina lake na kupata leseni na hivi hutosha kuanza kufanya biashara.

Hasara kubwa ya kipekee ya muundo huu wa biashara ni kuwa mmiliki anabeba majukumu kwa madeni yote ya biashara yake. Hivyo ikiwa atapata matatizo ya kifedha, wadeni wanaweza kufungua kesi/ madai dhidi yake na yakifanikiwa yeye binafsi atawajibika kulipa madeni hayo kutoka kwenye vyanzo binafsi vya fedha.

Ubia
Hii ni biashara inayotambulika kisheria inayofanywa na watu wawili au zaidi wanaoshiriki katika umiliki, utendaji na faida au hasara za biashara hiyo. Ziko aina kuu mbili za ubia, ubia wa jumla (usio na ukomo wa madeni) na ubia wenye ukomo wa madeni.

Katika ubia usio na ukomo wa madeni (ubia wa jumla), wabia wanaendesha biashara na wanawajibika kwa madeni ya biashara na mali zao binafsi zinaweza kulipia madeni hayo. Kwenye ubia wenye ukomo wa madeni, baadhi ya wabia huwa na ukomo wa kuwajibika kwa madeni ya biashara na baadhi huwa hawana. Wale wasio na ukomo wa kuwajibika kwa madeni ya biashara wanamiliki biashara na wanawajibika binafsi kwa madeni ya biashara, na wale wenye ukomo huwekeza tu, hawana nguvu ya moja kwa moja katika maamuzi ya biashara na hawawajibiki kuchangia fedha binafsi kulipa madeni ya biashara.

Uwajibikaji binafsi wa wabia kwa madeni ya biashara ni suala kubwa la kufikiria iwapo unatazamia kuendesha biashara kwa mfumo wa ubia. Kama ilivyo kwa wafanyabiashara wanaomiliki biashara peke yao, wabia wanawajibika kwa fedha zao binafsi kulipia madeni ya biashara. Kila mbia wa jumla (asiye na ukomo wa madeni) anaweza kufanya maamuzi na kuingia katika makubaliano ambayo wabia wenzake wote watayaheshimu na yatawaathiri (kutegemeana na makubaliano/ mkataba wa ubia wao) kwa niaba ya biashara.

Kumbuka kuwa biashara ya ubia ina gharama kubwa zaidi kuianzisha na kuiendesha kuliko biashara ya mtu binafsi, hii inatokana na ukweli kuwa kuna taratibu mbalimbali inabidi zifuatwe kabla ya biashara kuanza. Taratibu hizo ni pamoja na kuweka makubaliano ya namna ya kuendesha biashara, mgawanyo wa mapato na mengine mengi.

Ikiwa utaamua kuendesha biashara kwa mfumo wa ubia, hakikisha kuwa umeweka kimaandishi makubaliano au mkataba kuonesha namna maamuzi yatakavyofanyika, namna ya kumaIiza tofauti zinazotokea katika kufanya maamuzi, na hata namna ya kufikia makubaliano ya kubadilisha umiliki wa biashara itakapohitajika kufanya hivyo. Makubaliano hayo yanasaidia sana pale itakapotokea kwa sababu moja au nyingine biashara imeingia katika matatizo ya kifedha au ya kiuendeshaji, au ikitokea mbia mmojawapo anataka kuondoka kwenye biashara.

Mkataba wa ubia unapaswa kukazia kuhusu kusudi la biashara na mamlaka na wajibu wa kila mbia. Ni vema kupata msaada wa kisheria kutoka kwa mwanasheria mwenye uzoefu na mambo ya biashara ndogo na za kati katika kuandika mkataba wa ubia. Mambo mengine ambayo ni muhimu yazungumziwe katika makubaliano ya ubia ni:

Umiliki utachangiwa kwa viwango gani? Si lazima viwango vya umiliki na na mgawanyo wa majukumu vilingane kati ya wabia wote. La msingi ni kuhakikisha kiwango cha kila mmoja kiko katika makubaliano.

Maamuzi yatafanyika kwa mtindo gani? Ni vema kuweka makubaliano juu ya haki za kupiga kura baina ya wabia ikiwa wameshindwa kufikia muafaka kwenye suala fulani. Ikiwa wabia ni wawili tu na umiliki wao ni nusu kwa nusu, uko uwezekano wa kushindwa kufikia muafaka katika kuamua jambo. Kuepusha hili, biashara zingine huamua kuweka mbia wa tatu, mtu anayeaminika na kummilikisha asilimia ndogo tu ya biashara, ili kusaidia kuiondoa biashara kwenye mkwamo wa aina hiyo.

Ikiwa mbia mmoja atajiondoa, kiasi cha kumlipa kitaamuliwaje? Namna mojawapo ya kuamua kuhusu hili ni kuwa na mhusika aliye nje ya ubia, mfano benki, au mhasibu kutafuta mtathmini atakayethaminisha kiasi cha kumlipa mbia anayejitoa katika ubia.

Ikiwa mbia atajitoa katika biashara, ni lini anapaswa kulipwa fedha yake? Hii inaweza kuwekwa katika makubaliano ili ijulikane bayana. Ikiwa itachukua muda mrefu, inaweza kuwa busara kuweka makubaliano kuwa ilipwe pamoja na riba. Bila makubaliano haya uendeshaji biashara unaweza kuathirika ikiwa mtu atajitoa na kiasi chote kulazimika kulipwa kwa mkupuo kwa haraka mara anapojitoa. Kampuni yenye ukomo wa madeni

Kampuni yenye ukomo wa madeni ni muundo wa shirika ambamo uwajibikaji wa wamiliki (wanahisa) kwa madeni ya biashara unakomea kwenye kiasi walichowekeza katika kampuni, au ambacho wamekubaliana kukiweka dhamana kwa ajili ya kampuni. Hivyo kampuni yenye ukomo wa madeni inaweza kuwa na ukomo kwa njia ya hisa au ukomo kwa njia ya dhamana waliyoweka wanahisa. Suala la nani anaweza kuwa mwanahisa wa kampuni binafsi linatawaliwa na sheria na kanuni za kampuni.

Kama ilivyo kwa biashara zingine zinazoendeshwa hapa nchini, Kampuni yenye ukomo wa madeni inapaswa kusajiliwa na Mamlaka ya Usajili na Leseni za Biashara, ambayo iko chini ya wizara inayohusika na Biashara. Katika usajili, hatua ya kwanza ni kupata kibali cha kutumia jina la biashara kinachotolewa na mamlaka hiyo. Nyaraka/ taarifa zifuatazo zinahitajika katika mchakato wa kuanzisha kampuni:

Jina la kampuni (ambalo lazima lipitishwe na msajili wa makampuni);

Anuani rasmi ya ofisi ya kampuni Tanzania;

Majina, anuani, na utaifa wa wanahisa wa kwanza na wakurugenzi wa kampuni (angalau wawili kwa kampuni binafsi au saba kwa kampuni ya umma).

Mkataba wa kuanzisha kampuni (unaotaja madhumuni ya kampuni) na sheria/ makubaliano yanayosimamia utendaji na maamuzi ya kampuni (inayotaja muundo wa uongozi na michakato ya maamuzi mbalimbali). Angalau nakala mbili za kila waraka zinapaswa kuwasilishwa.;

Kujaza fomu maalumu zenye tamko kuwa kampuni imezingatia matakwa ya sheria ya makampuni Tanzania; na

Kulipa tozo/ ada za kuwasilisha nyaraka, usajili, na ushuru wa stempu.
Ahsanteni..

kumbuka kuwasiliana nasi kwa ushauri zaidi 0766865041

Unataka kuanzisha biashara,jiunge nasi.....

Kwa ushauri na matangazo wasiliana nasi kwa 0766865041


Biashara yoyote huanza na wazo, ila wazo pekee halitoshi, linahitaji kufanyiwa kazi. Hapo ndipo watu wengi huweza kuanza kujisikia kuzidiwa. Si ajabu kuona mtu anakatishwa tamaa kwa kutizama msururu wa mambo yanayohitajika ili kuanzisha biashara, lakini pia kuanzisha biashara ni rahisi kuliko unavyodhani. Kama ilivyo katika lengo lolote kubwa, ukianza kwa kutengeneza malengo madogo madogo ya kutekeleza utaweza kufanya mambo yote muhimu katika kuanzisha biashara.
Jinsi ya Kuanzisha Biashara Ndogo

Kuanzisha na kuendesha biashara inahitaji msukumo, nia na kipaji. Inahitaji pia utafiti na mipango. Kama ilivyo kwenye mchezo wa drafti, mafanikio kwenye biashara ndogo huanza na maamuzi sahihi katika hatua za mwanzoni. Ikumbukwe pia hapa kuwa pamoja na kwamba makosa madogomadogo ya mwanzoni yanaweza yasiue biashara yako, inahitaji ujuzi, nidhamu, na bidii kuyasahihisha.
Ili kuboresha uwezekano wa kufanikiwa, unapaswa kutenga muda wa kujichunguza na kutathmini malengo yako kibiashara na malengo binafsi. Tumia taarifa hiyo kutengeneza kwa umakini mkubwa mpango wa biashara ambao utakuwezesha kufikia malengo yako.

Mchakato wa kuandaa mchanganuo wa biashara utakuchochea kufikiria hata baadhi ya mambo ambayo usingekumbuka kuyafikiria katika hali ya kawaida. Mchanganuo wako utakuwa zana muhimu sana unapopambana kutafuta fedha kwa ajili ya biashara yako. Mchanganuo huo pia unaweza kutumika kama kigezo cha kila mara kufuatilia/ kupima mafanikio ya biashara yako.
Yako mambo kadhaa yanayohitajika katika biashara yoyote.

Jambo la kwanza kabla ya kuanzisha biashara ni kuwa unatakiwa ujiulize sababu za wewe kutaka kuingia kwenye biashara. Sababu zilizozoeleka za kuanza biashara ni:

Unataka kujiongoza mwenyewe.
Unataka uhuru wa kifedha.
Unataka uhuru wa kutumia ubunifu wako.
Unataka kutumia kikamilifu ujuzi na ufahamu wako
Jambo la pili ni kuamua biashara ipi inakufaa? Ili kufahamu ni biashara ipi inakufaa, jiulize maswali yafuatayo:
Ninapenda kutumiaje muda wangu?
Nimejifunza au kusomea ujuzi gani?
Watu wengine wanazungumzia ubora wangu kwenye mambo gani?
Nina muda kiasi gani kuendesha biashara kwa ufanisi?
Katika mambo ninayopendelea yapo ambayo yanaweza yakawa fursa ya biashara?
Biashara yangu itahudumia sehemu/ kundi gani katika soko?
Je? Wazo langu linatekelezeka na litakidhi hitaji katika soko?
Ushindani nilionao ni upi? Nami nina uwezo gani katika ushindani?
Biashara yangu ina manufaa gani kuzidi zingine zilizopo?
Je? Naweza kutoa huduma zenye ubora zaidi?
Je? Naweza kutafuta soko kwa ajili ya bidhaa/ huduma zangu?
Ukishapata majibu ya maswali hayo hapo juu ni wazi kuwa utakuwa ulishaanza kujua ni biashara gani unaweza kuianzisha. Lakini pia unatakiwa ujiulize maswali haya hapa ili kuwa na uhakika na biashara ambayo utaifanya.

Ninakusudia kuanzisha Biashara gani?
Nitauza bidhaa gani au nitatoa huduma gani? Biashara nitafanyia eneo gani?
Nitatumia ujuzi na uzoefu gani kwenye biashara?
Biashara yangu itakuwa na muundo gani kisheria?
Niiite biashara yangu jina gani?
Nitatumua vifaa gani, na nitakuwa na mahitaji gani?
Nahitaji bima ya aina gani?
Nahitaji fedha kiasi gani?
Nina rasilimali zipi?
Nitajilipaje?

Majibu yako yatasaidia kutengeneza mpango makini, uliofanyiwa utafiti wa kutosha, ambao utautumia kama ramani ya kuelekeza kila hatua katika utekelezaji wa biashara na hata kupata mtaji.
Chagua muundo sahihi wa biashara yako.
Unapoanzisha biashara yoyote, mojawapo ya maamuzi muhimu sana ya kufanya ni uchaguzi wa muundo wa hiyo biashara. Mambo yanayozingatiwa katika kuchagua muundo wa biashara ni pamoja na:

Masharti ya kisheria
Uwajibikaji wa wamiliki kwa madeni ya biashara
Aina ya shughuli za biashara
Mgawanyo wa mapato
Mahitaji ya mtaji
Idadi ya wafanyakazi na utawala
Manufaa na hasara za kihasibu/ kikodi
Urefu wa mzunguko wa biashara

SIRI YA UTAJIRI

Kwa ushauri wa kibiashara wasiliana na 0766865041,joseph

Watu wengi wanajiuliza, "Siri ya utajiri ni nini?" Jee ni mbinu gani
zinaweza kumsaidia mtu kupata utajiri? Siri kubwa ya utajiri ni
kujifunza elimu ya namna ya kutafuta mtaji, kuwekeza kwa busara kwa
namna ambayo daima panakuwa na ziada na faida. Kwa bahati mbaya
sana, elimu hii haifundishwi darasani ila wanayo wafanyabiashara
wachache na kila anayefanikiwa kujifunza siri hii huwa tajiri na
huendelea kuificha.

Kwa bahati nzuri, katika utafiti wagu nimeweza
kuigundua siri ya utajiri. Kwa kuwa ninapenda wasomaji wangu waweze
kufanikiwa na wapate manufaa kwa kununua kitabu hiki nimeamua
kuiweka siri hii wazi:-

- Siri ya kwanza ya kuelekea ukwasi ni kubuni mradi endelevu,
yaani unaoweza kuitoa ziada na faida.
- Siri ya pili ya kuelekea kwenye utajiri ni kujifunza na
kujenga tabia ya kuweka akiba
- Siri ya tatu ni kuwekeza fedha hizo za akiba katika vitega
uchumi ambavyo vinazalisha faida endelevu.
- Siri ya nne ni kujifunza namna ya kufanya biashara na
kuanzisha biashara yako ili iwe indelevu.

Kuna njia mbili za namna ya kupata utajiri zenye uhakika. Njia ya
kwanza ni njia ndefu ambapo wataalamu na watafiti wa masuala ya
fedha wameigundua njia hii ni rahisi kuifuata kwa sababu haihitaji
uwe na kipato kikubwa, wanashauri kwamba ujenge tabia ya kuweka
akiba, anza kuweka akiba ya T.shs 1,000 kila siku sawasawa na TShs
30,000 kwa mwezi, matokeo yake ni kwamba kama utaweka akiba yako kwa
kipindi cha miaka 65 bila riba yoyote utakuwa na akiba TSshs
23,725,000 (Milioni Ishirini na Tatu Mia Saba Ishirini na Tano
Elfu).

Kama utawekeza fedha hiyo na kupata riba ya asilimia 10% kwa
kila mwaka itazaa na kukuletea TShs 2,750,000,000 (Bilioni Mbili na
Milioni Mia Saba Hamsini). Hesabu hii inaweza ikakutisha na usiamini
macho yako lakini hiyo ni siri ya nguvu ya hesabu na riba kama
alivyozielezea mwanafizikia Enstein kwamba katika dunia hii hakuna
kitu chenye nguvu kama hesabu za riba.

Pengine njia hii inaweza kuwa
ni ndefu sana na ya kukatisha tamaa. Wengi wetu hatuwezi kusubiri
muda mrefu. Hivyo tungependa kuwa na mafanikio ya kiuchumi kwa
haraka. Lakini nasisitiza kama kipato chako ni kidogo anza leo
kuweka akiba ya TShs 1,000 kwa siku.

Dundulizo la akiba hii hukutiririshia utajiri bila wewe kukusudia
kwani utaweza kukidhi hitajiko la ghafla kama kuugua safari ya
dharura gharama za likizo na hata kutumia mbinu hii kama mpango wa
elimu kwa watoto wako iwapo utawaanzishia hivi mara tu kila
mmojawapo anapozaliwa au unaweza kuutumia kama upanga wa siku zijazo
kwa mirathi ukianza hivyo leo kwa kupangilia namna hiyo kwa kila
kusudio lako la baadaye.

Hebu tuangalie njia ya pili.

- Njia ya pili ya mkato ni kuongeza kiwango cha kuweka akiba kama
wewe ni mtu mwenye shughuli za kuzalisha ziada. Kipato chako
kinaweza kuwa kinaongezeka kila mara. Badala ya kuweka akiba ya TShs
1,000 kwa siku jiwekee malengo ya kuweka akiba ya TShs 10,000.

Anza kwa kutenga asilimia 10% ya mapato yako hadi utakapofikia lengo la
TShs 10,000 au zaidi kwa siku. Badala ya lengo lako kutimia kwa
miaka sitini na tano (65) litatimia haraka zaidi. Kwa mfano ukiweka
akiba ya TShs 10,000 kwa siku kwa muda wa miaka sita na miezi sita
bila riba yoyote utapata TShs. 23,725,000. Ukiwekeza fedha hiyo na
kupata riba ya asilimia 10% kwa miaka sita na miezi sita utapata
TShs. 33,917,505.78. Kama fedha hiyo utaendelea kuweka akiba kwa
riba hiyohiyo hadi kufikia muda wa miaka kumi utapata TShs.
63,112,201.43.

Kwa kuwa kitu cha muhimu hapa ni kuweka akiba na kuwekeza akiba hiyo
katika kitegauchumi chenye kutoa faida kubwa, utajiuliza jee uwekeze
kwenye kitega uchumi chenye kutoa faida kiasi gani? Wataalamu wa
mambo ya fedha wanashauri kuwa uwekeze fedha yako kwenye
kitegauchumi chenye kutoa faida ya angalau asilimia 10% Kwa mfano
unaweza kuwekeza kwenye Akaunti ya TAJIRIKA ya Standard Chatered
Bank" inatoa riba ya asilimia kumi 10% pia unaweza kuwekeza kwa
kununua hisa katika soko la hisa na mitaji.

Kwa wastani wa watafiti wa masuala ya fedha viwango vya mapato
yatokanayo na hisa kwa gawio pamoja na kukua kwa mtaji ni zaidi ya
asilimia 11% ambayo ni makubwa kwa kiwango cha kawaida cha asilimia
kumi (10%).

Baada ya kueleza siri ya namna ya kupata utajiri nitazitaja njia
zingine ambazo zinaweza kukuwezesha kuwa tajiri.

1. Unaweza kurithi mali na fedha kutoka kwa wazazi wako. Hii ni
njia ya kubahatisha kwani watu matajiri siyo wengi na hivyo watoto
wenye bahati kama hii ni wachache pia.

2. Unaweza kusomea ujuzi au utaalamu katika fani yenye malipo
mazuri na kujiajiri mwenyewe. Kwa mfano, unaweza kusomea fani kama
ya Uanasheria, Uhasibu na Udaktari au ufundi / sanaa na kadhalika.

3. Unaweza kuanzisha biashara yako na kuiendesha ili kupata
ziada kubwa.

4. Unaweza kuendeleza vipaji vyako na kuwa mwanamichezo au
msanii wa kulipwa.

5. Unaweza kutunga vitabu juu ya suala lolote unalolijua. Kwa
mfano, kama wewe ni mtu uliyebobea katika masuala ya muziki unaweza
kutunga kitabu kinachofundisha watu namna ya kuwa mwanamuziki.
Watunzi wengi wa vitabu ni matajiri wakubwa. Hii ni kazi unayoweza
kuifanya mara moja lakini ukavuna matunda yake kwa muda mrefu sana.

6. Unaweza kuwa mbunifu na kuanza kuuza mawazo yako au kutumia
chombo ulichokibuni kukuingizia fedha.

7. Unaweza kucheza bahati nasibu na kushinda. Tatizo hapa soko
na wateja wa aina hii ya huduma ni haba. Hiki ni kitu cha
kubahatisha na nimekitaja makusudi ili kuwapa onyo wasomaji kwani
watu wengi wanapenda sana kucheza michezo ya kubahatisha.
Uwezekano wa kutajirika kwa njia hii ni mdogo sana.

Hivyo,
nawashauri wasomaji kuachana na njia hii ya kutafuta utajiri.
Nawashauri wachague njia yoyote inayofaa na inawezekana kwa
kufuatana na mazingira yanayomzunguka mtu husika. Mkulima au mfugaji
anaweza kuzingatia fani hii na kutajirika sana. Kwa kweli hakuna
mipaka, hasa hapa kwetu Tanzania kwa sababu ya wingi wa fursa za
kuweza kujishughulisha na kuwa tajiri.

Maelezo ya kina juu ya aina ya biashara au mbinu unaweza kuzitumia
kutafuta na kupata faida utayapata katika sehemu ya pili ya kitabu
hiki.

Inawezekana kuwa tofauti kati ya mtu tajiri na mtu maskini inatokana
na kile tulichojifunza kutoka kwa wazazi wetu. Wazazi maskini
huwaambia watoto wao wajitahidi kusoma sana ili wapate maksi nzuri
darasani na ili baadaye waweze kupata kazi nzuri. Wakati wazazi
matajiri huwapa watoto wao elimu ya namna ya kutafuta fedha.

Kwa kawaida tukiwa shuleni tunapewa ripoti ya masomo. Katika maisha
tunatakiwa kuwa na ripoti yetu ya maisha nayo ni orodha ya mali
tulizonazo ikiwa ni pamoja na elimu ya kuzaliwa na ya kusomea na
fedha taslimu zile zilizo katika hifadhi mbalimbali.

Kwa kufuata tafsiri ya Umoja wa mataifa mtu masikini ni yule ambaye
kipato chake hakizidi TShs 1,000 kwa siku.

Inawezekana kuwa mfumo wa kifedha wa mtu maskini ni mfumo ambao
humfanya kutumia kipato chake chote kulipia matumizi huwa hana ziada
wala uwezo wa kuweka akiba hana madeni na hana mali.

Mfumo wa fedha wa mtu mwenye kipato cha kati ni mfumo ambao humfanya
kuwa na mali kama magari, nyumba na kadhalika. Mara nyingi mali hizo
huwa zinapatikana kwa mikopo na hutumia mshahara kulipia matumizi
na madeni, hasa kama madeni ni makubwa, mtu mwenye kipato cha kati
anapaswa kumuona mshauri wa maswala ya biashara.

Hatua anazoweza kuchukua ili kujikwamua na tatizo la madeni anaweza kulazimika kuuza
baadhi ya mali zake ambazo amezinunua kwa kutaka kuonyesha ufahari
tu na ambazo hazina umuhimu. Kwa mfano kama mtu ana magari matatu ya
kutembelea, anaweza kuuza magari mawili kubaki na gari limoja na
fedha atakayoiokoa kuiwekeza au kutumia kama mataji na kuanzisha
biashara ili kujiongezea kipato.

Mfumo wa mtu tajiri ni mfumo ambao unamwezesha kuwa na biashara
yake, kumiliki mali nyingi, kuwa na fedha nyingi katika akiba na awe
ameziwekeza kwenye vitega uchumi vinavyolipa faida kubwa zaidi ya
asiliamia kumi, kama vile nyumba za kupangisha na hisa. Mtu huyu
hana wasiwasi na maisha. Anaweza kusafiri au kuugua lakini
vitegauchumi vyake vinaendelea kumwingizia fedha. Siri kubwa ya
matajiri ni uwezo wa kutumia fedha na kuziwekeza kupata faida kubwa.

Hiki ni kitabu cha vitendo. Yote unayoyasoma humu inabidi uyafanyie
kazi ili yakusaidie. Tofauti kati ya maskini na tajiri iko katika
kuchukua hatua. Tajiri hujifunza mambo ya kumwendeleza na kuchukua
hatua kwa kutekeleza kwa vitendo yale anayojifunza na anayoyaona
yanaweza kumuinua kiuchumi. Maskini huwa anajifunza mambo na
kuyaacha kichwani bila kuchukua hatua au kuyafanyia kazi
aliyojifunza na hivyo fursa ya kupata utajiri inampita hivihivi. Kwa
hiyo, kama unataka kuwa tajiri anza mara moja kufanya yafuatayo:-

1. Anza kuweka akiba ya T.Shs 1,000 kila siku. Tengeneza
kisanduku na tumbukiza TShs. 1,000 kila siku. Zikifika TShs. 50,000
kafungue akaunti ya TAJIRIKA, kwenye Benki ya "Standard Chatered".
Kisha endelea kuweka TShs. 30,000 kila mwezi. Jinsi mapato yako
yatakavyokuwa yanaongezeka tenga asilimia kumi (10%) ya mapato yako
uweke akiba kila mwezi.

Lengo lako liwe ni kuweka TShs 10,000 au
zaidi kila mwezi. Fedha unayoweka ni kama unapanda mbegu. Kumbuka
hii ndiyo hatua ya kwanza kuelekea kwenye utajiri. Faida katika
benki hii ni kubwa. Inaanzia asilimia 6.5% kwa kianzio cha TShs.
50,000 hadi TShs. 5,000,000 na asilimia 10% kwa kiwango kinachozidi
TShs. 10,000,000. Fedha utakazoziweka huko usiziguse mpaka ukiona
zimekuwa nyingi ndipo utaamua na kupanga ukaziwekeze sehemu gani.

2. Jifunze pia mbinu za kutafuta fedha.

Njia rahisi ni ya uhakika ya kukuwezesha kufanikiwa kiuchumi katika maisha ni kutafuta
mshauri au mtaalamu anayejua mbinu za uongozi wa biashara ili
akushauri vizuri juu ya yale unayonuia kutekeleza.

3. Inawezekana pia bado hujawa na biashara ya aina yoyote.
Kama ndivyo anza kufanya utafiti kuona utafanya biashara gani.

Mawazo ya biashara gani ufanye unaweza kuyapata katika sehemu ya
pili ya kitabu hiki. Kila mara hakikisha unatenga asilimia 10% ya
mapato yako na kuweka kwenye akaunti yako ya TAJIRIKA. Kumbuka
kwamba kuwa na biashara yako ni siri ya pili ya kuelekea kwenye
kupata utajiri. Kama unayo biashara yako unaweza kumtafuta mtaalamu
wa biashara kuangalia jinsi unavyoweza kuiboresha au kuipanua.

4. Panga malengo ya muda wa mwaka mmoja miaka mitano na miaka
ishirini ili kuhakikisha kwamba unajikomboa kiuchumi. Malengo yako
makuu yawe ni:- kuwa na akiba ya fedha za kutosha katika akaunti
yako , kuwa na biashara yako, na vitega uchumi vya aina tofauti
ambavyo unaweza kuvisimamia vizuri.

5. Kama wewe ni mwajiriwa, kipimo chako cha mafanikio kiwe ni
kujiuliza swali, kama utaacha kazi yako ya mshahara utaweza kuishi
kwa kutumia kipato chako cha pembeni kwenye biashara yako kwa muda
gani? Mafanikio yako yatakuja pale utakapoweza kutumia kipato chako
cha ziada bila kutegemea mshahara, na hapo ndipo unaweza kuacha kazi
na kwenda kuimarisha biashara zako au kuendelea na kazi huku pia
ukijiimarisha kibiashara.

6. Kama utafuata mpango wa namna hii na kujituma kwa juhudi na
maarifa kwa muda wa miaka mitano (5) unaweza kuwa tajiri na maisha
yako yanaweza kuwa mazuri.